Topic

Uandishi Wa Barua

Estimated reading: 2 minutes 1681 views Contributors

Summary: Barua za kirafiki ambazo pia huitwa za kidugu huandikwa baina ya watu wa undugu au jamii moja. Katika mada hii utaweza kujifunza muundo wa uandishi wa barua ya kirafiki na jinsi ya kuandika barua ya kirafiki. Utaweza kutofautisha kati ya barua ya kirafiki na ile isiyokuwa ya kirafiki.

Barua za Kirafiki

Iwapo ni katika ndugu barua za kirafiki zaweza kuwa kwa watu kama: baba, mama, shangazi, mume, mke, mtoto, na kadhalika. Katika jamii waandikiwao barua za kirafiki ni kama jirani, rafiki, mpenzi, mwalimu, mwanafunzi, daktari, mgonjwa, na kadhalika.

Muundo wa Barua za Kirafiki

Elezea muundo wa barua za kirafiki

Mambo muhimu ya kuzingatia katika uandishi wa barua za kirafiki:

  • ANWANI kamili ya mwandishi, katika herufi hukaa juu upande wa kulia mwa karatasi.
  • TAREHE, chini ya anwani.
  • MTAJO wa heshima kwa anayeandikiwa, kama vile, mpendwa, mpenzi, na kadhalika, huandikwa kushoto, baada ya tarehe.
  • UTANGULIZI wa barua yenyewe ambao kwa desturi huwa ni salamu.
  • BARUA YENYEWE ambayo ndiyo kiini cha waraka.
  • SALAMU za kumalizia, pengine kwa jamaa na jamii.
  • HITIMISHO, katika aya, maalumu ambayo huwa, kwa mfano: ‘Ni mimi baba yako akupendaye,’ na kadhalika.
  • SAHIHI ambayo si sharti wala muhimu sana.
  • JINA au MAJINA ya mwandishi, mwishoni.

Tazama mfano wa barua ya kirafiki:

Example 1

MUSOMA FISH PACK

S.L.P 4546

MUSOMA

23/5/2013

Mwanangu Nyamchele,

Ninafuraha kukujulisha kuwa nimepokea barua yako. Mambo yote uliyoyaeleza nimeyaelewa barabara. Huku nyumbani sote tu wazima na ni matumaini yetu kwamba afya yako ni nzuri.

Tabia ya kulalamikia chakula ni mbaya. Tabia kama hii ikikomaa husababisha ulafi. Kumbuka hukwenda shuleni kula kama nguruwe. Huko shuleni nimekupeleka ili usome kwa bidii na ujifunze mengi. Usitamani kustarehe na kufikiria maakuli na anasa zingine za ulimwengu huu. Ondoa fikira za chakula akilini mwako na uache uzembe, eboo!

Hebu nikuonye kuhusu kuwapima na kuwachagua walimu. Walimu katika shule hiyo ni wabobezi na ndio maana nikakupeleka hapo. Wanajua mnayostahili kufundishwa. Huna ruhusa ya kusema eti walimu wengine ni wakali na hufundisha haraka haraka sana. Wewe unahitaji kutega sikio na kutii. Ukiwa makini na uwe na imani utayaelewa mambo unayofundishwa. Usisahau kuwa mchagua jembe si mkulima.

Mambo makubwa unayostahili kuyatilia bidii ni masomo yako. Muda wa miaka minne ni mfupi sana. Uonyeshe adabu njema kila wakati. Uwaonyeshe walimu wako taadhima na uwatii daima dawamu.

Jambo lililo kubwa katika shughuli yoyote ni uvumilivu. Ukivumilia utavuna matunda mabivu. Sitachoka kukusisitizia, ‘Ukilima pantosha, utavuna pankwisha.’ Fanya kila jitihada utimize mambo mengi iwezekanavyo kuanzia leo lakini usipapie chochote. Ndo ndo ndo hujaza ndoo.

Mungu akubariki. Umwombe akusaidie katika kila jambo. Ujiepushe na maovu yoyote yale. Ukiwa na jambo usiwe na hofu kutuarifu mara moja. Mama yako amekusalimu sana. Amenikumbusha nikupashe hakuna refu lisilo na ncha.

Kwaheri kwa sasa.

Ni mimi, baba yako akupendaye,

Magafu Malima

Test Your Knowledge

Click below to generate a short, interactive 5-question quiz based on this lesson.

No comments yet — be the first to share your thoughts.

Leave a Comment

Share this Doc

Uandishi Wa Barua

Or copy link

CONTENTS

Mathematics Form Five Teacher’s Guide TIE Book PDF Download – New Syllabus

Delivering high-quality Advanced Level instruction requires structured lesson pl

Mathematics Form Five and Form Six BAM TIE Book PDF Download -New Syllabus

Navigating non-mathematical Advanced Level subject combinations still requires a

Mathematics Form Five TIE Book PDF Download – New Syllabus

Transitioning into Advanced Level secondary education introduces a significant r

Mathematics Form Six TIE Book PDF Download – New Syllabus

Completing your final year of Advanced Level secondary education demands rigorou

Mathematics Form Six

Form Six Mathematics builds directly on the foundations established in Form Five

Mathematics Form Five

Transitioning to Advanced Level (A-Level) Mathematics form five requires masteri

Kitabu cha Historia ya Tanzania na Maadili Kidato cha Sita New Syllabus PDF (TIE)

Kufikia mwaka wa mwisho wa masomo yako ya sekondari ya juu (A-Level) ni hatua ku

Kitabu cha Historia ya Tanzania na Maadili Kidato cha Tano PDF (TIE)

Kuingia Kidato cha Tano katika mchepuo wa masomo ya sanaa na jamii kunahitaji ma

Kitabu cha Historia ya Tanzania na Maadili Kidato cha Pili New Syllabus PDF (TIE)

Kama unatafuta njia rahisi na ya haraka ya kufanya vizuri kwenye masomo yako, Ki

Kitabu cha Historia ya Tanzania na Maadili Kidato cha Kwanza TIE New Syllabus PDF

Kama ndio unaanza safari yako ya elimu ya sekondari na unataka kuelewa vizuri as

Kitabu cha Fasihi ya Kiswahili Kidato cha Sita TIE PDF (Mtaala Mpya ACSEE)

Kufikia Kidato cha Sita katika masomo ya Fasihi ya Kiswahili kunahitaji maandali

Kitabu cha Kiswahili Kidato cha Sita TIE PDF (Mtaala Mpya ACSEE)

Unapofikia hatua ya mwisho ya masomo yako ya sekondari ya juu, kuwa na zana sahi

Chat Icon Close Icon

Subscribe

×
Cancel