Topic

Uhakiki Wa Kazi Za Fasihi Andishi

Estimated reading: 96 minutes 6033 views Contributors

Summary: Fasihi andishi ni tawi la fasihi linalotumia sanaa ya maneno kufikisha ujumbe kwa hadhira kwa njia ya maandishi. Zipo aina nyingi za fasihi andishi, miongoni mwa hizo ni pamoja na hadithi fupi, riwaya, tamthiliya na mashairi.

Fani katika Ushairi wa Wasakatonge

Mwandishi: Taasisi ya Kiswahili, Zanzibar
Wachapishaji: Oxford University Press
Mwaka: 2001

Jina la Kitabu

Jina la kitabu Wasakatonge linasadifu yaliyomo ndani yake. Maudhui yanayoelezwa yanagusa jamii ya sasa, ikiwemo masuala ya maadili, siasa, uchumi, na ukombozi wa kiutamaduni. Pia inajadili changamoto na suluhisho la matatizo yanayoikumba jamii, hivyo jina la kitabu linaendana na maudhui yake. Kifani, Malenga wapya wameweka muundo na mtindo wa kisasa unaovutia.

Muundo

Katika hakiki ya muundo wa ushairi, tunaangalia idadi ya mistari katika ubeti. Ubeti unaweza kuwa na mistari miwili, mitatu, minne, na kuendelea. Aina za muundo zimepewa istilahi maalum ili kutofautisha aina moja na nyingine. Mfano:

Tathlitha:
Mashairi yenye mistari mitatu kwa kila beti. Mengi ya mashairi haya ni ya kisasa. Mfano ni shairi la “Hali Halisi”, “Puuzo”, “Ua”, “Kuunge”, na “Tunzo”.

Shairi la Ua:
“Ua limejituliza mtini laning’inia,
Mwenyewe laniliwaza, furahani lanitia,
Ua sasa limepea, macho walikodolea.”

Tarbia:
Mashairi yenye mistari minne kwa kila beti. Mfano ni shairi la “Kitendawili”, “Mkulima”, “Majonzi”, “Bahari”, “Samaki Mtungoni”, “Kifungo”, na mengine mengi.

Shairi la Kifungo:
“Miaka imeshapita, sasa najiamkia,
Naanza bila kusita, bahati kujitafutia,
Hapo nitapoipata, mola jishukuria,
Kifungo kimenichosha, minyororo nafungua.”

Takhmisa:
Mashairi yenye muundo wa mistari mitano katika kila ubeti. Mfano ni mashairi ya “Siharakie Maisha” na “Israfu”.

Shairi la Israfu:
“Mali ulojichumia,
Ni yako nakubalia,
Lakini kiangalia,
Vipi unaitumia,
Mwenzangu nakuusia israfu haifai.”

Sabilia:
Mashairi yenye mistari kuanzia sita na kuendelea. Mfano ni shairi la “Punda” na “Pasua Uwape Ukweli”.

Shairi la Punda:
“Toka ulipozaliwa, maishayo ni kizogo,
Hujapata kuenziwa, waishi tiriigivyogo,
Nawe hujajielewa, u kiumbe hu kigogo,
Kama ungefadhiliwa, usingebeba mzigo,
Hakika ulionewa, hustahili kipigo,
Haki umeitambua, idadi japo kidogo.”

Mtindo

Imetumika mitindo ya aina zote mbili, ya kisasa na ya kimapokeo.

Mtindo wa Kisasa:
Mtindo ambao haufuati kanuni za urari wa vina na mizani katika beti. Huitwa pia mashairi huru. Mfano wa mashairi yaliyotumia mtindo wa kisasa ni “Pasua Uwape Ukweli” na “Haki”.

Mtindo wa Kimapokeo:
Mtindo huu hufuata kanuni na sheria zote za vina na mizani katika utunzi wake. Mara nyingi huwa na mistari minne katika kila ubeti. Mashairi mengi yaliyotumia mtindo huu ni ya kimapokeo.

Katika Wasakatonge, matumizi ya mitindo hii miwili yanaonyesha ubunifu wa Malenga wapya na uwezo wao wa kuwasilisha ujumbe kwa njia mbalimbali, ili kuvutia wasomaji wa rika zote na kuendana na mabadiliko ya nyakati.

Mfano wa mashairi yaliyotumia mtindo wa kisasa ni mashairi ya“Pasua uwape ukweli”, “Haki” “Payuka

Screen Shot 2016 07 27 at 16.13.08 1469625248191

Pia mfano wa mashairi ya kimapokeo ni shairi la“Mkulima”, “Bahari”, “Tuyazingatie haya” “Nipate wapi mwingine”.

MATUMIZI YA LUGHA

Diwani ya malenga wapya imetumia lugha yenye ubunifu bora wa kisanaa.Vilevile ni lugha rahisi na sanifu inayoeleweka kwa hadhira lengwa.

Tamathali za Semi

  • Tashibiha:“Nizikwe kama wezangu, nisitupwe kama paka” –Shairi la“Nini wanangu”.“Hata pamoja muweko, ubaguzi umezama,kama nguzo” –Shairi la“Tunzo ubeti wa nne”.“Mfanowe kama radi, chini inapoanguka”.-Shairi la“Nipate wapi mwingine”.“Nikabaki kama ng’onda” –Shairi la“Nipatieni dawa”.“Maisha ni kama njia”-Shairi la“Maisha ni kama njia”.“Yameotewa na kombe, mithili gome la mti”-Shairi la“Bahari ubeti wa pili”.
  • Tashihisi:“Ewe ulimi sikia” –Shairi la“Ulimi”.“Haki wa tutisha,tusikuandame,kwa matendo yetu” –Shairi la“Haki ubeti wa kwanza”.“Njiwa ameishanitoka, nipate wapi mwingine”-Shairi la“Nipate wapi mwingine”.“Samaki wasikitika, kudai walikotoka, Wote wamekasirika, uhuru wanachotaka,”-Shairi la“samaki mtungoni”.
  • Sitiari:“wamejipa uwezo wa Rabuka” – “Mpaka lini”“Paka shume jigeuza” – “Kwanini?”“mshumaa ” – “Hali halisi”

Mbinu nyingine za kisanaa

  • Onomatopea/ tanakali sauti:“kokoriko”- “Mkulima”“Parakacha” – “kwanini”.
  • Takriri:“Charuka” – “charuka”
  • Tashititi:“Nasikia mnatunga mwatungani washairi?” “mwabwaja mwasema nini”

Matumizi ya semi

  • Methali:“Simwamshe asilani aliyelala usingizini” – “Payuka”“Fahali wapiganapo, nyasi ndio huumia”- “Sokomoko baharini”“Subira yavuta heri”- “Siharakie maisha”

Matumizi ya taswira

  • “Samaki” – wanyonge – “samaki mtungoni”
  • “Ua” – mpenzi – “Ua”
  • “Punda”-wanyonge – “Punda”
  • “Mvuvi” – wanyonyaji – “Samaki mtungoni”
  • “Njiwa” – mpenzi – “Nipate wapi mwingine”
  • “Baharini” – nchi – “Sokomoko”
  • “Abiria”- wananchi –“Sokomoko”

Leave a Comment


Share this Doc

Uhakiki Wa Kazi Za Fasihi Andishi

Or copy link

CONTENTS

Thrive! English Standard Four PDF-Free Download

Do you want to see your primary school student express themselves with absolute

Excel Now! Hisabati Darasa La Tatu PDF [Download Bure]

Je, unatafuta njia rahisi ya kumsaidia mwanafunzi wako kufanya vizuri na kupenda

Thrive! Civic and Moral Standard Three PDF [Free Download]

Looking for the official TIE Civic and Moral Standard Three textbook? Access thi

Thrive! English Standard Three PDF-Free Download

Looking for the official TIE English Standard Three textbook? Grab this free dig

Learn with Joy: Social Studies Standard Three PDF Free

Need the official TIE Social Studies Standard Three textbook? Get the free digit

Ignite Curiosity! Download the Official Standard 3 Science Technology Book Free

Looking for the official TIE Science and Technology Standard Three textbook? Gra

Master Mathematics Standard Three Textbook PDF [Free Download]

Need the Mathematics Standard Three textbook? This free PDF follows the Tanzania

English Standard Five

Are you looking for the English Standard Five textbook for primary schools in Ta

Standard Seven

Excel! Social Studies Standard Four PDF [Free Download]

Need the Social Studies Standard Four textbook? This free PDF follows the Tanzan

Thrive! Civic and Moral Education Standard Four PDF Free

Download Civic and Moral Education Standard Four book PDF. Covers TIE syllabus t

Standard Six

Chat Icon Close Icon

Subscribe

×
Cancel