Comment

Topic

Uundaji Wa Maneno

Estimated reading: 4 minutes 108 views

Kutumia Uambishaji

Kubainisha Mofimu katika Maneno

Bainisha mofimu katika maneno

Uambishaji wa maneno ni kitendo cha kupata maneno kwa kubandika Mofimu kwenye kiini cha neno, uambishaji kutokea kabla ya kiini cha neno au mzizi wa neno. Mfano kiini pig- unaweza kuunda maneno kama inapiga, anayepiga, mpigaji, amepigika nk.

Mofimu zinazobadilika kwenye kiini cha neno huitwa Viambishi.

Katika lugha ya Kiswahili viambishi hutokea kabla na baada ya kiini cha neno.

Mfano

Wanapendana = Wa-na-pendan-a kiini cha neno ni-pend-.

Mofimu zilizobadilisha baada ya kiini –an-na-a viambishi vinavyotokea kabla ya kiini cha neno huitwa viambisha awali au tangulizi. Viambisha vinavyotokea baada ya kiini cha neno huitwa viambishi tamati au fuatishi.

Example 1

Angalia mifano ifuatayo:

NenoViambisha AwaliKiiniViambisha Tamati
Unapendeleau-na--penda-el-e-a
Waliongozanawa-li--ongoz-an-a
Analimaa-na--lim--a
anayeiimbishaa-na-ye-imb--ish-a

Dhima za Mofimu

Bainisha dhima za mofimu

Baadhi ya dhima za uambishaji ni kama ifuatavyo:

  1. Kuonyesha upatanisho wa usanifu maana ya maneno yanayozalishwa kutofautiana katika msingi wa kusanifu tu, lakini uhusiano wa maneno hayo hutokana na kiini au mzizi wake uleule.Mfano;Fundisha kiini chake ni fund. Unaweza kuzalisha maneno mengine kwa kutumia mzizi/kiini kilichopo kama vile fundishana, mafundisho, mfundishaji, fundishwa, fundishana.
  2. Uambishaji huonyesha nafsi
  3. Uambashaji huonyesha njeo (muda)
  4. Uambishaji huonyesha urejeshi
  5. Uambishaji huonyesha ukanushi
  6. Uambishaji huonyesha hali mbalimbali za kitenzi

Vitenzi vikiambishwa huweza kujenga/kuunda/kuzalisha vitenzi vingine au nomino.

Example 2

Mfano

VitenziKiiniNominoVitenzi
Cheza-chez-Mchezaji, mchezowanacheza/atamchezea
Piga-pig-Mpigaji, Mpiganajiwatanipiga, aliyempiga/wanaompiga

Uambishaji hutumika kuzalisha viwakilishi na vielezi.

Neno (Kiwakilishi)KiiniKielezi
Huyu, HuyoHuHumu, humo
Wangu, wako, wakewa
Hii, hizo, hikihi

Viambishi awali vina dhima ya kudokeza nafsi, njia, idadi urejeshi na ukanushi.Mfano: Hawakulima

  • Ha-, kiambishi cha ukanushi
  • Ku-, kiambishi njeo/wakati

Viambishi tamati vina dhima mbalimbali hudokeza hali ya utendekaji, ukamilishaji au kimalizio cha neno na kauli za matendo kama vile kutendwa, kutendewa,kutendeka nk.

Dhima:Ukanusho, kutendeana, agizo na mtendwa, ukamilisho, usababishi.

Example 3

Mfano

NenoViambishi Tamati
Anapiga-a
Wanapigana-an
Asipigwe-w
Amempigisha-ish-

Viambishi tamati vina dhima ya kutambulishwa mapema/nomino zilizoundwa kutokana na vitenzi.

NenoKiiniViambishi Tamati
Pigapig--o
Mchezochez--o
Mtembezitembe--z-i
Mfiwa-fi--us-a

Kutumia Mnyumbuliko

Mazingira yanayosababisha Mahitaji ya Maneno Mapya

Elezea mazingira yanayosababisha mahitaji ya maneno mapya

Mnyumbulisho ni neno linalotokana na neno nyumbua. Kunyumbua kitu ni kuvuta, kuongeza urefu wa kitu hicho.

Kunyumbua katika lugha ya Kiswahili ni kuongeza vinyumbulishi katika katika kiini ili kupata msamiati mpya. Hivyo basi, mnyumbulisho ni njia mojawapo na inasaidia kuunda maneno kwa njia ya kunyumbulisha.

Viambishi vinapochukuliwa katika kiini cha neno, basi neno hilo huwa limenyumbulishwa. Kwa mfano neno lima kiini chake lim- huweza kunyumbulishwa na kupata maneno mengine mpya, kama lim-ishwa, lim-ia, lim-w-a.

Pia maneno ya mnyumbulisho yanaweza kuundwa kwa kuongeza viambishi kwenye shina, kwa mfano:

NenoKiiniShinaManeno ya Mnyumbuliko
ElekeaelekelekaElekeana, elekea, elekwa, elekesha
ShikishanashikshikishaShikishana, shikisha, shikishaneni

Kwa ujumla tunawaza kusema kuwa maneno ya kawaida hunyumbulika. Hivyo kiini/mzizi au shina moja huweza kuzalisha maneno mengine mengi ambayo yanatokana na msingi mmoja wa maana.

Dhima ya Uambishaji na Mnyambulikoa wa Maneno

Fafanua dhima ya uambishaji na mnyambulikoa wa maneno

Dhima ya uambishaji ni kuleta upatanisho wa kisarufi, kuonesha idadi na umoja na wingi katika ngeli za majina, kuonesha njeo na kuonesha urejeshi pamoja na hali mbalimbali kwa uambikaji wa viambishi kabla ya mzizi wa neno. Aidha dhima ya mnyambuliko ni kuonesha matokeo ya tendo na kuzalisha kauli mbalimbali kwa kupachika viambishi baada ya mzizi wa neno.

Kuunda Maneno mbalimbali kwa kutumia Mnyambuliko

Unda maneno mbalimbali kwa kutumia mnyambuliko

Uundaji wa maneno mbalimbali kwa kutumia mnyambuliko hufanyika kwa kupachika viambishi baada ya mzizi wa neno na hivyo kulifanya neno husika liweze kuonesha matokeo mbalimbali ya matendo pamoja na kuzalisha kauli mbalimbali za matendo.

Activity 1

Unda maneno mbalimbali kwa kutumia mnyambuliko

Kutumia Maneno ya Mnyambuliko katika Miktadha mablimbali

Tumia maneno ya mnyambuliko katika miktadha mablimbali

Maneno ya mnyambuliko hutumika katika miktadha mbalimbali ambapo miktadha hiyo hujitokeza katika kauli mbalimbali za vitenzi. Kauli hizo ni kauli ya kutenda, kauli ya kutendwa, kauli ya kutendewa, kauli ya kutendea, kauli ya kutendeka, kauli ya kutendesha, kauli ya kutendana, na kauli ya kutendama.

Activity 2

Tumia maneno ya mnyambuliko katika miktadha mbalimbali

Share this Doc

Uundaji Wa Maneno

Or copy link

CONTENTS

Translation And Interpretation | English Form 5 & 6

Translation is a process by which ideas that are written in one language ar...

Writing Skills | English Form 5 & 6

Are the abilities that allow you to write effectively and concisely. A competent...

Reading Skills | English Form 5 & 6

Reading is the process of going through written information or piece of wor...

Speaking Skills | English Form 5 & 6

What is Speaking? SPEAKING SKILLS: Speaking is simply the act of talking wh...

Listening Skills | English Form 5 & 6

Listening is ability to accurately receive and interpret messages in the communi...

Word Formation | English Form 5 & 6

This is the field or branch of morphology which studies different principles or ...

Introduction To Language | English Form 5 & 6

Language is a symbol system based on pure or arbitrary  conventions…...

Topic

Form Five and Form Six

Ecology

Ecology is the study of the interactions between living things, such as humans, ...

Evolution

EVOLUTION Evolution is  a change in the genetic composition of a population...

Genetics

Genetics is the study of heredity and variationHeredity- is the passage of chara...

Chat Icon Close Icon

Subscribe

×
Cancel