Comment

Topic

Uhakiki Wa Kazi Za Fasihi Andishi

Estimated reading: 96 minutes 1281 views

Summary: Fasihi andishi ni tawi la fasihi linalotumia sanaa ya maneno kufikisha ujumbe kwa hadhira kwa njia ya maandishi. Zipo aina nyingi za fasihi andishi, miongoni mwa hizo ni pamoja na hadithi fupi, riwaya, tamthiliya na mashairi.

Fani katika Ushairi wa Mashairi ya Chekacheka

Hakiki fani katika Ushairi wa Mashairi ya Chekacheka

MWANDISHI: THEOBALD A. MVUNGI

WACHAPISHAJI: EDUCATIONAL PUBLISHERS AND DISTRIBUTORS LTD.

MWAKA: 1995

MUUNDO

Mwandishi ametumia muundo wa tarbia, mashairi yake yote yamefuata muundo huu. Beti za mashairi yake zina mistari minne. Mengi ya mashairi yake, mistari imegawanyika katika vipande viwili yaani mistari ina vina vya kati na vya mwisho. Mfano katika shairi la “Mashairi ya “Ngulu”;

Pia katika baadhi ya mashairi yake ameyaumba katika kipande kimoja, yaani yana kina cha mwisho tu. Mfano ni mashairi kama vile ya“Dhahabu ya fahari”, “Utu umekuwa kima”,“Seng’enge”mfano katika shairi la“Utu umekuwa kima”

MTINDO

Mtindo aliotumia mwandishi ni mtindo wa kimapokeo kwani amezingatia vigezo vya vina na mizani katika utunzi wa mashairi yake. Mfano katika shairi la”“Tuambae ukasuku”

MATUMIZI YA LUGHA

  • Tashibiha:“Mshairi jihadhari, usishikwe kama fimbo.” – “Tuambae ukasuku.”“Na wasiothaminiwa, wapimwao kama nyasi”- “Raia si mali kitu”“Mapenzi yasinadiwe, kama shati dukani” – “Penzi lisilo heshima”“Utaliwa kama pumba” – “Utaliwa kama pumba”“Kaburu si mtu hata, kwake sisi sawa punda” – “Utumwa huru”.“Pungufu akili yake, mla punje kama kuku” – “Tuambaeukasuku
  • Tashihisi:“Mejaribu kujongea, ndege awe mkononi,Yeye juu hurukia, namuomba samahani.” – “Njiwa kiumbe mtini”“Moyo nimeshauri, lakini umekaidiMoyo kiburi hatari, mfanowe kama radiMoyo mefumbata shari, unayakwepa marudi,Moyo u mwilini mwangu, jirudi tuwe pamoja.” – “Moyo”Nipishe wewe senge’nge” – “Seng’enge”.“Kijiji kisichoringa” – “Mashairi ya Ngulu”.“Akili yamsaliti, kikongwe haoni kweli.”- “ Ni wapi ushauri?”
  • Sitiari:“Mshairi awe Nyati”- “Tuambae ukasuku”“Sisi ni miamba gogo”- “Raia si mali kitu”“Ile chai kikombeni, rangi yake Mwafrika” – “Chai”.“Kwetu ulikuwa mama” – “Indira”“Utu umekuwa kima” – “Utu umekuwa kima”“Uroho umekujaa, watu mefanya kondoo” – “Utaliwa kama pumba”

Matumizi ya semi

  • Misemo:“Fedha fedheha” – “Chanzo cha huo uozo”
  • Methali:“Akishaoza samaki, busara ni kumtupa” – “Chatu mmeza matonge”
  • Nahau:“Wabunge waote meno, wasivilambe viatu” –wawe na mamlaka– “Tuambae ukasuku”Mbinu nyingine za kisanaa
  • Takriri:“Chai ninaipa hati, kwa kutukidhia haja,Chai imewekwa kati, kwetu sisi sote waja,Chai majani ya miti, hii miti yenye tija.” – “Chai”Neno“njiwa” limejirudia katika kila ubeti –“Njiwa”Neno “moyo” limerudiwa katika kila ubeti. – “Moyo”Neno “mauti” limejirudia katika ubeti wa kwanza – “Utaliwakamapumba”Neno “Ngulu” katika mashairi ya “Ngulu”.

Ujenzi wa Taswira

Matonge”- madaraka-“Mwinyi umewasha moto”Nyati”– watawala –“Tuambae ukasuku”“Mfugaji”– mwananchi – “Tuambae ukasuku”“Jiko”– madaraka “Kuna nini huko jikoni”“Chatu”– watawala –“Chatu mmeza matonge”“Chura”– mtu asiye na msimamo – “Chura umegundulika”

Leave a Comment


Share this Doc

Uhakiki Wa Kazi Za Fasihi Andishi

Or copy link

CONTENTS

Translation And Interpretation | English Form 5 & 6

Translation is a process by which ideas that are written in one language ar...

Writing Skills | English Form 5 & 6

Are the abilities that allow you to write effectively and concisely. A competent...

Reading Skills | English Form 5 & 6

Reading is the process of going through written information or piece of wor...

Speaking Skills | English Form 5 & 6

What is Speaking? SPEAKING SKILLS: Speaking is simply the act of talking wh...

Listening Skills | English Form 5 & 6

Listening is ability to accurately receive and interpret messages in the communi...

Word Formation | English Form 5 & 6

This is the field or branch of morphology which studies different principles or ...

Introduction To Language | English Form 5 & 6

Language is a symbol system based on pure or arbitrary  conventions…...

Topic

Form Five and Form Six

Ecology

Ecology is the study of the interactions between living things, such as humans, ...

Evolution

EVOLUTION Evolution is  a change in the genetic composition of a population...

Genetics

Genetics is the study of heredity and variationHeredity- is the passage of chara...

Chat Icon Close Icon

Subscribe

×
Cancel