Comment

Topic

Uhakiki Wa Kazi Za Fasihi Andishi

Estimated reading: 96 minutes 1282 views

Summary: Fasihi andishi ni tawi la fasihi linalotumia sanaa ya maneno kufikisha ujumbe kwa hadhira kwa njia ya maandishi. Zipo aina nyingi za fasihi andishi, miongoni mwa hizo ni pamoja na hadithi fupi, riwaya, tamthiliya na mashairi.

Fani katika Tamthiliya ya Watoto wa Mama N’tiliye

Mwandishi: Emmanuel Mbogo
Wachapishaji: Heko Publishers
Mwaka: 2002

Jina la Kitabu

Jina la kitabu Watoto wa Mama N’tiliye linasadifu yaliyomo ndani ya kitabu. Kinaeleza kuhusu maisha ya watoto wa mama ntilie, maisha ya dhiki, umaskini uliokithiri, na mazingira yasiyo ya faraja yaliyokosa malezi bora, chakula bora, elimu, na huduma ya afya. Jina hili linaakisi yaliyomo ndani ya kitabu na hali halisi katika jamii yetu, ambapo akina mama wengi wanakabiliana na changamoto za kifedha huku wakiwa na jukumu la malezi. Mwandishi ametumia jina hili ili kuibua kero na matatizo yaliyoko katika jamii.

Utangulizi wa Kitabu

Riwaya ya Watoto wa Mama N’tiliye inasadifu maisha ya Mtanzania wa leo. Inaangazia masuala ya umaskini, hali ngumu ya maisha, wimbi la watoto wa mitaani, masuala ya uhalifu, wizi, na ujambazi, pamoja na malezi. Mwandishi Mbogo amejitahidi sana katika fani kwa kutumia muundo na mtindo unaovutia wasomaji na kuumba wahusika kwa usadifu wa hali ya juu huku mandhari yake ikisawiri maisha ya Tanzania.

Muundo

Muundo uliotawala katika riwaya hii ni muundo wa rukia au rejea. Mwandishi anatuelezea visa mbalimbali kwa njia ya kurukia matukio na kurudi nyuma kwa wakati. Mfano, katika sura ya tatu mwandishi anaelezea safari ya Mama Ntilie kwenda Matombo (uk.34), kisha anaacha kisa hicho na kuelezea kuzaliwa kwa watoto Kurwa na Doto. Vilevile, mwandishi anadokeza safari ya Musa (uk.80) na Zita kupandwa na kichaa (uk.81). Riwaya imegawanywa katika sura tano, na visa na matukio yamejengwa katika muundo unaotegemeana ili kukamilisha kilele cha masimulizi.

Mtindo

Mtindo uliotumika ni wa masimulizi ya mjazo au lugha ya nathari. Mwandishi ameueleza visa mwenyewe na vingine wahusika wamevielezea. Pia ametumia mitindo kadhaa, kama vile:

  • Nafsi ya Tatu (wingi na umoja): “Peter aliokota kipande cha muhogo” (uk.15), “watu walisongamana walisukumana” (uk.26).
  • Nafsi ya Kwanza (umoja na wingi): “nitasema nitasema!” (uk.58), “twende tule” (uk.56).
  • Nafsi ya Pili (dayalojia): Majibizano kati ya Mama Ntilie na Zita (uk.89).

Matumizi ya nafsi mbalimbali yanavuruga monotoni na kuvuta umakini wa msomaji, huku nyimbo na majibizano yakiburudisha na kuongeza mvuto wa masimulizi.

Matumizi ya Lugha

Riwaya imetumia lugha rahisi, fasaha, na inayoeleweka kwa wasomaji. Kuna matumizi ya lugha ya Kiingereza (uk.36, “chloroquine”, “faster faster mama”), na lugha ya mitaani (uk.41, “kudeku”). Tamathali za semi zimetumika sana:

  • Tashibiha: “mdomo wake ulio kaa kama bakuli la pombe” (uk.10), “miguu kama ya mamba” (uk.15).
  • Tashihisi: “mabega yenyewe tayari yalikuwa yamechongwa kwa pombe ya gongo” (uk.10), “moshi wenye harufu ya kuudhi ulilelea hewani” (uk.19).
  • Sitiari: “Nyama nyie” (uk.10).
  • Ritifaa: “Mama? Mama yuko wapi, Baba yuko wapi?” (uk.38).
  • Tafsida: “haja kubwa” (uk.91).

Mbinu nyingine za kisanaa kama onomatopea, takriri, mjalizo, mdokezo, nidaa, na matumizi ya semi (nahau, methali, misemo) zimeongeza uhalisia na mvuto katika riwaya hii.

Wahusika

Mama Ntilie

  • Mama mzazi wa Peter na Zita
  • Mke wa Mzee Lomolomo
  • Mlezi mzuri wa familia
  • Mvumilivu na mwenye huruma
  • Mchapakazi na anayejituma
  • Ana hali ngumu kimaisha

Mzee Lomolomo

  • Mume wa Mama Ntilie
  • Baba wa Peter na Zita
  • Mlevi na mvivu
  • Si mlezi bora, hajali familia
  • Anakufa kwa sababu ya kunywa pombe sana

Peter

  • Mtoto wa Mama Ntilie
  • Anakosa elimu kwa sababu ya umaskini
  • Ana bidii na mchapakazi
  • Ana huruma
  • Anafungwa jela kwa kufanya biashara haramu ya madawa ya kulevya

Zita

  • Mtoto wa kike wa Mama Ntilie
  • Anakosa elimu kwa sababu ya umaskini
  • Mchapakazi
  • Anagombana na Kurwa, hakupenda aje kwao, roho mbaya
  • Anakufa kwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa

Doto

  • Mtoto yatima wa mtaani
  • Anauawa baada ya kujiingiza katika uhalifu wa wizi
  • Mgomvi na katili

Kurwa

  • Ndugu yake Doto
  • Anaishi mtaani, yatima
  • Ana huruma, nguvu, na jasiri
  • Mchapakazi
  • Anaishia jela kwa makosa ya Musa na Peter

Musa

  • Mtoto aliyekosa elimu baada ya kukosa sare na ada
  • Alikosa malezi mazuri ya wazazi
  • Mhalifu, anafanya biashara haramu za madawa ya kulevya
  • Ana tamaa ya pesa
  • Rafiki mbaya kwani alimshauri Peter kuuza madawa ya kulevya

Mwalimu Chikoya

  • Mwalimu wa Peter na Zita
  • Aliwafukuza Peter na Zita shule kwa kukosa ada
  • Si mwalimu mzuri

Mandhari

Mandhari iliyotumika ni ya jiji la Dar es Salaam, kwa kutajwa maeneo kama Manzese, Tabata, Kiwanda cha Urafiki, Kisutu, na Muhimbili. Pia kuna mandhari ya nyumbani kwa Mama Ntilie (uk.5), hospitali ya Muhimbili (uk.89), na jaani-jaa la Tabata (uk.20). Mandhari haya yanasaidia kuibua dhamira halisi zinazosawiri maisha ya Mtanzania wa leo, kama vile umaskini na wimbi la watoto wa mitaani.

Leave a Comment


Share this Doc

Uhakiki Wa Kazi Za Fasihi Andishi

Or copy link

CONTENTS

Translation And Interpretation | English Form 5 & 6

Translation is a process by which ideas that are written in one language ar...

Writing Skills | English Form 5 & 6

Are the abilities that allow you to write effectively and concisely. A competent...

Reading Skills | English Form 5 & 6

Reading is the process of going through written information or piece of wor...

Speaking Skills | English Form 5 & 6

What is Speaking? SPEAKING SKILLS: Speaking is simply the act of talking wh...

Listening Skills | English Form 5 & 6

Listening is ability to accurately receive and interpret messages in the communi...

Word Formation | English Form 5 & 6

This is the field or branch of morphology which studies different principles or ...

Introduction To Language | English Form 5 & 6

Language is a symbol system based on pure or arbitrary  conventions…...

Topic

Form Five and Form Six

Ecology

Ecology is the study of the interactions between living things, such as humans, ...

Evolution

EVOLUTION Evolution is  a change in the genetic composition of a population...

Genetics

Genetics is the study of heredity and variationHeredity- is the passage of chara...

Chat Icon Close Icon

Subscribe

×
Cancel