Comment

Topic

Uhakiki Wa Kazi Za Fasihi Andishi

Estimated reading: 96 minutes 1285 views

Summary: Fasihi andishi ni tawi la fasihi linalotumia sanaa ya maneno kufikisha ujumbe kwa hadhira kwa njia ya maandishi. Zipo aina nyingi za fasihi andishi, miongoni mwa hizo ni pamoja na hadithi fupi, riwaya, tamthiliya na mashairi.

Uhakiki wa Fani katika Tamthiliya ya “Kilio Chetu”

Mwandishi: Medical Aid Foundation
Wachapishaji: Tanzania Publishing House (TPH)
Mwaka: 1996

Jina la Kitabu

Kilio Chetu ni jina linaloasadifu yaliyomo katika kitabu. Masuala kama upotofu wa maadili kwa vijana kama Suzi na Joti, mimba za utotoni, na madhara ya ugonjwa hatari wa UKIMWI ni kweli kilio chetu na kilio cha Taifa zima. Kitabu hiki kinaonyesha changamoto za maadili katika jamii na linaashiria umuhimu wa kubadilika.

Utangulizi wa Kitabu

Kilio Chetu ni tamthiliya inayozungumzia maisha ya Suzi na Joti, watoto wadogo wanaoingia katika mapenzi kutokana na ukosefu wa elimu ya kijinsia. Inafafanua athari za UKIMWI na mtazamo wa wazazi kuhusu elimu ya jinsia kwa vijana wao. Tamthiliya hii inabeba ujumbe wa mabadiliko na kuwakomboa vijana kutokana na janga la UKIMWI.

Muundo

  • Sehemu ya Kwanza: Inaonyesha jinsi UKIMWI unavyoathiri jamii.
  • Sehemu ya Pili: Inaeleza athari za UKIMWI, kifo cha Fausta, na Suzi kugundulika kujihusisha na mapenzi.
  • Sehemu ya Tatu: Inaeleza juu ya watoto kama Joti na Suzi wanaoanza mapenzi katika umri mdogo na madhara ya utandawazi.
  • Sehemu ya Nne: Inasimulia tabia hatarishi za Joti na jinsi Ana anavyopingana na vishawishi kwa msaada wa elimu ya jinsia.
  • Sehemu ya Tano: Suzi anagundulika kuwa na mimba ya Joti na kujuta sana.
  • Sehemu ya Sita: Inaonyesha jinsi Joti alivyopata magonjwa kutokana na UKIMWI na umuhimu wa kumtunza mgonjwa wa UKIMWI.

Mtindo

Tamthiliya hii imetumia mitindo mbalimbali, ikiwemo:

  • Dayalojia: Majibizano kati ya wahusika.
  • Mianzo na miisho ya kifomula: Mfano, “paukwa… pakawaa… Niendelee… nisiendelee?”
  • Utambaji: Mwandishi anasimulia matukio moja kwa moja.
  • Matumizi ya nafsi ya pili: Majibizano ya watu wawili au zaidi.
  • Matumizi ya tanzu za fasihi: Mfano, nyimbo na methali.

Wahusika

  • Suzi: Binti mdogo wa darasa la sita, anajihusisha na mapenzi, hana msimamo, na anapata mimba.
  • Joti: Kijana mdogo anayejihusisha na wasichana wengi, hana elimu ya jinsia, na anaathirika na kufa kwa UKIMWI.
  • Mama Suzi: Anashikilia ukale, hataki mabadiliko, na hakumpa Suzi elimu ya jinsia.
  • Baba Joti: Mkali, anatumia viboko kuelimisha, na si mwaminifu katika ndoa yake.
  • Anna: Binti mdogo mwenye elimu ya jinsia, anashinda vishawishi, na anatoa elimu kwa vijana wenzake.
  • Baba Anna: Anatoa elimu ya jinsia, ni mlezi bora, na anafaa kuigwa na jamii.
  • Mjomba: Kaka yake Mama Suzi, anatoa elimu ya jinsia na UKIMWI, na anapinga mila potofu.
  • Mama Joti: Anapambana na matatizo ya ndoa, na anafahamu umuhimu wa elimu ya jinsia.
  • Jirani: Ana imani potofu za kishirikina, anaamini UKIMWI ni laana.
  • Chausiku: Msichana wa mtaani, anajihusisha na mapenzi na vijana na watu wazima.
  • Chogo, Mwarami na Jumbe: Marafiki wa Joti, wana tabia mbaya, na hawafai kuigwa na jamii.

Mandhari

Mandhari iliyotumiwa na mwandishi ni ya mjini, ikionyesha maisha ya mijini kama uwanja wa Sabasaba, lugha ya mtaani, na matatizo kama utandawazi na picha za ngono.

Matumizi ya Lugha

  • Ubunifu wa kisanaa: Lugha rahisi na inayoeleweka kwa hadhira lengwa.
  • Matumizi ya lugha nyingine: Kiingereza na lugha za kikabila.
  • Matumizi ya lugha ya mtaani: Mfano, “mshefa” na “mshikaji” (rafiki), “kamba” (kudanganya), “vidosho” (wasichana).
  • Tamathali za semi: Tashibiha, tashihisi, sitiari, tafsida, mubaalagha.
  • Mbinu za kisanaa: Tanakali sauti, tashtiti, takriri.
  • Semi: Methali, nahau, misemo.

Matumizi ya Taswira

  • Dubwana: Ugonjwa wa UKIMWI.
  • Nguru: Aina ya samaki wabaya, kufananishwa na mtu mbaya.
  • Kinyago: Kumfananisha Suzi na kitu kisicho na thamani.

Kwa ujumla, tamthiliya ya Kilio Chetu ni kazi yenye mtazamo wa kimabadiliko, inayotumia fani na maudhui kuibua masuala muhimu katika jamii, hasa katika vita dhidi ya UKIMWI na upotovu wa maadili.

Leave a Comment


Share this Doc

Uhakiki Wa Kazi Za Fasihi Andishi

Or copy link

CONTENTS

Translation And Interpretation | English Form 5 & 6

Translation is a process by which ideas that are written in one language ar...

Writing Skills | English Form 5 & 6

Are the abilities that allow you to write effectively and concisely. A competent...

Reading Skills | English Form 5 & 6

Reading is the process of going through written information or piece of wor...

Speaking Skills | English Form 5 & 6

What is Speaking? SPEAKING SKILLS: Speaking is simply the act of talking wh...

Listening Skills | English Form 5 & 6

Listening is ability to accurately receive and interpret messages in the communi...

Word Formation | English Form 5 & 6

This is the field or branch of morphology which studies different principles or ...

Introduction To Language | English Form 5 & 6

Language is a symbol system based on pure or arbitrary  conventions…...

Topic

Form Five and Form Six

Ecology

Ecology is the study of the interactions between living things, such as humans, ...

Evolution

EVOLUTION Evolution is  a change in the genetic composition of a population...

Genetics

Genetics is the study of heredity and variationHeredity- is the passage of chara...

Chat Icon Close Icon

Subscribe

×
Cancel