Comment

Topic

Uhakiki Wa Kazi Za Fasihi Andishi

Estimated reading: 96 minutes 1287 views

Summary: Fasihi andishi ni tawi la fasihi linalotumia sanaa ya maneno kufikisha ujumbe kwa hadhira kwa njia ya maandishi. Zipo aina nyingi za fasihi andishi, miongoni mwa hizo ni pamoja na hadithi fupi, riwaya, tamthiliya na mashairi.

Hakiki ya Fani katika Riwaya ya “Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe”

Jina la Kitabu: Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe

Mwandishi: Edwin Semzaba
Wachapishaji: Nyambari Nyangwine Publishers
Mwaka: 2006

Utangulizi wa Kitabu

“Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe” ni tamthiliya maarufu sana ambayo imewahi kuigizwa katika redio Tanzania na katika majukwaa mbalimbali hapa nchini. Ni tamthiliya ambayo imeundwa vyema katika vipengele vya fani na maudhui. Mwandishi ametumia lugha nzuri na yenye mvuto kwa wasomaji, yenye mbinu za kifasihi zilizosheheni, na muundo wenye mtiririko mzuri unaoakisi kuanza kuchipuka kwa matukio mpaka kilele cha matukio. Wahusika wamebeba vyema uhusika wao, mfano Ngoswe.

Ameteua dhamira zinazogusa jamii ya leo kama vile uzembe, madhara ya ulevi, uzembe kazini, na suala la matabaka kati ya mjini na vijijini. Mtazamo, falsafa, na msimamo wa mwandishi ni kulenga kuibadilisha jamii na kuleta maendeleo.

Jina la Kitabu

Jina la kitabu “Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe” linasawiri vyema yaliyomo ndani ya kitabu hicho, kwani Ngoswe ndiye mhusika mkuu anayebeba dhamira kuu ya tamthiliya. Penzi limeonekana kuwa ni kitovu cha uzembe kwani ndilo lililopelekea kuteketezwa kwa karatasi za takwimu za sensa. Hivyo, jina la kitabu si tu kwamba linasawiri yaliyomo katika kitabu bali pia katika jamii.

Mtindo

Mwandishi ametumia mtindo wa dayalojia au majibizano. Mwandishi amepanga visa na masimulizi kwa kutumia majibizano ya wahusika.

  • Matumizi ya Nafsi ya Kwanza: Mwandishi ndiye ameyafafanua na kuelezea baadhi ya matukio. Katika karibu kurasa zote, mwandishi ameonekana kuwa ndiye msimuliaji wa matukio.
  • Matumizi ya Nafsi ya Pili: Hapa watu wawili na zaidi wanajibizana. Wahusika wanajibizana kuibua dhamira na migogoro. Kuna majibizano baina ya Mzee Mitomingi, Ngoswe, na Mazoea, nk.

Muundo

Muundo uliotumika ni muundo wa moja kwa moja au sahili, ambapo matukio yanaoneshwa kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Mwandishi amepanga visa na matukio yake katika maonesho matano. Kila kichwa kina maelezo yaliyojadiliwa katika onesho hilo.

  1. Kijito: Hapa yanaeleza jinsi mambo yanavyoanza, jinsi Ngoswe anavyoingia kijijini, anavyopokelewa, na kuanza kufahamiana na wenyeji wake.
  2. Vijito: Ngoswe anaanza kufanya kazi iliyompeleka kijijini na tunaanza kuoneshwa changamoto anazokumbana nazo.
  3. Mto: Ni mwendelezo wa matukio ya mwanzo ambapo visa vinazidi kukua.
  4. Jito: Ngoswe anakumbana na changamoto nyingi zaidi katika kazi yake. Anaanguka kwa sababu ya kujiingiza katika mapenzi na msichana Mazoea, anaendekeza ulevi, na kuharibu kazi kabisa.
  5. Bahari: Inaoneshwa mwisho wa mambo jinsi yalivyokuwa. Yanaonekana mahojiano baina ya Serikali, Ngoswe, na Mitomingi juu ya uzembe uliofanyika wa kupoteza takwimu na hapa ndipo suluhisho linapotolewa juu ya matatizo hayo.

Wahusika

Ngoswe

  • Kijana wa kiume mwenye umri kati ya miaka 20-25
  • Ameelimika na amestaarabika
  • Anatumwa na serikali kufanya sensa kijijini
  • Anajihusisha na mapenzi na msichana Mazoea
  • Ni mlevi na hana umakini katika kazi
  • Aliharibu kazi ya serikali
  • Hafai kuigwa na jamii

Mazoea

  • Msichana mwenye umri kati ya miaka 18-20
  • Binti wa Mzee Ngengemkeni Mitomingi
  • Hana elimu na hajastaarabika
  • Ana nidhamu ya woga na tama
  • Hana msimamo; alikubali kuchukuliwa na Ngoswe hali akijua alishatolewa mahari
  • Hafai kuigwa na jamii

Ngengemkeni Mitomingi

  • Balozi katika kijiji chake
  • Baba mzazi wa Mazoea
  • Ameoa ndoa ya mitara, ana wake wawili
  • Hajaelimika
  • Anashikilia mila na desturi za kale
  • Mlevi na mkali sana
  • Anateketeza karatasi za takwimu

Wahusika Wengine

  • Mzee Jimbi: Mwanakijiji, hajaelimika, ni mlevi, ana wake wawili, anashikilia ukale
  • Mama Mazoea: Mke mkubwa wa Mitomingi, mama yake Mazoea, mlezi wa familia, hapewi nafasi ya kutoa maamuzi katika familia
  • Mama Inda: Mke wa pili wa Mzee Mitomingi, mama yake Huzuni, hapewi nafasi ya kutoa maamuzi, ni mlezi wa familia

Mandhari

Mandhari ya tamthiliya hii imechorwa katika mazingira ya kijijini. Mambo yanayoelezwa ni ya kijijini kama vile kilimo, hali ya watu kimaisha, huduma duni za kijamii kama vile shule, na umbali wa makazi toka nyumba moja hadi nyingine. Mandhari hii inaibua dhamira mbalimbali kama vile umaskini, ukosefu wa elimu, huduma duni za afya vijijini, na masuala ya imani potofu.

Matumizi ya Lugha

Mwandishi ametumia lugha fasaha na rahisi kueleweka kwa wasomaji. Pia kuna matumizi ya lugha nyingine kama vile “bell bottom” (uk. 1).

  • Matumizi ya Semi:
  • Methali: “Penye nia pana njia” (uk. 22), “Waona vyaelea vyaundwa” (uk. 27)
  • Misemo: “Akuwaniae ujovu haji kweupe” (uk. 14)
  • Nahau: “Hebu keti tutupe mawe pangoni” – tule chakula (uk. 11), “Mbongo zimelala” – ana maarifa (uk. 7), “Pombe na yeye ni pete na chanda” – anapenda pombe sana (uk. 14)
  • Matumizi ya Tamathali za Semi:
  • Tafsida: “Wala hajarudi, kama ingekuwa ni kujisaidia si angekuwa amekwishamaliza?” (uk. 21)
  • Tashbiha: “Vumbi jekundu kama ugoro wa subiana” (uk. 1), “Sarawili yake miguuni kama kengele ya bomani” (uk. 8), “Wanaondoka huku wakitazamwa kama vile mizuka” (uk. 17)
  • Sitiari: “Kiziwi mkubwa wee!” (uk. 7), “Pombe na yeye ni pete na chanda!” (uk. 14), “Karatasi? za takwimu? Ndio wanyama gani hao?” (uk. 26)
  • Mubaalagha: “Kupeleka chakula ndio umefanya makao!” (uk. 11), “Kujibu swali ndio ukachukua mwaka mzima!” (uk. 11)
  • Mbinu Nyingine za Kisanaa:
  • Mdokezo: “Sijui….. siwezi….. namuogopa baba” (uk. 22), “Huyo mtoto wenu wa kwanza anaishi hapa au…..” (uk. 16)
  • Takriri: “Mama Masikio! We Mama Masikio!” (uk. 9), “Hodi! Hodi!” (uk. 13), “Karibu karibu” (uk. 2)
  • Tashtiti: “Hivyo waitwa nani?” (uk. 5), “Mchumba? Kwani mchumba ni kitu gani?” (uk. 22), “Karatasi? Za takwimu? Ndio wanyama gani hao?” (uk. 26)
  • Onomatopea/Tanakali Sauti: Kifaruhande anacheka “Ha! ha! ha!” (uk. 7)

Ujenzi wa Taswira

Mwandishi ametumia taswira ya mto kuelezea visa vyake kwa mpangilio ufuatao:

  1. Kijito: Hapa mwandishi anaanza kueleza mambo yakiwa machanga kabisa, yanayoanza kuchipuka kama kijito kidogo ambacho ni sehemu ya mwanzo wa mto. Sehemu hii inafafanua jinsi Ngoswe anavyoingia kijijini na anavyoanza kufahamiana na wenyeji wake.
  2. Vijito: Huu ni muunganiko wa vijito vidogovidogo ambapo mwandishi anaanza kueleza visa vidogovidogo vinavyoungana na kujenga hadithi. Hapa Ngoswe anaanza kufanya kazi kijijini na tunaanza kuona changamoto anazokumbana nazo.
  3. Mto: Sehemu hii inaashiria kuwa mambo yameanza kuwa mazito zaidi, na visa vinaanza kukua. Ngoswe anazidi kuingia katika changamoto kubwa zaidi na matatizo yanazidi kumwandama.
  4. Jito: Hii ni taswira inayotumiwa kuashiria hatari kubwa zaidi. Mambo yamekuwa makubwa na magumu zaidi, na Ngoswe anakumbana na changamoto nyingi katika kazi yake. Anaanguka kabisa kwa sababu ya kujiingiza katika mapenzi na msichana Mazoea na kuendekeza ulevi, hivyo kuharibu kazi kabisa.
  5. Bahari: Hatimaye, mwandishi anaelezea hatima ya mambo. Ngoswe anazama na kupotea kabisa kama bahari yenye kina kirefu na maji mengi. Hafanikiwi kutoa takwimu kwani karatasi zilichomwa moto, hivyo kuonesha mwisho wa safari yake na kushindwa kwake kutekeleza majukumu.

Leave a Comment


Share this Doc

Uhakiki Wa Kazi Za Fasihi Andishi

Or copy link

CONTENTS

Translation And Interpretation | English Form 5 & 6

Translation is a process by which ideas that are written in one language ar...

Writing Skills | English Form 5 & 6

Are the abilities that allow you to write effectively and concisely. A competent...

Reading Skills | English Form 5 & 6

Reading is the process of going through written information or piece of wor...

Speaking Skills | English Form 5 & 6

What is Speaking? SPEAKING SKILLS: Speaking is simply the act of talking wh...

Listening Skills | English Form 5 & 6

Listening is ability to accurately receive and interpret messages in the communi...

Word Formation | English Form 5 & 6

This is the field or branch of morphology which studies different principles or ...

Introduction To Language | English Form 5 & 6

Language is a symbol system based on pure or arbitrary  conventions…...

Topic

Form Five and Form Six

Ecology

Ecology is the study of the interactions between living things, such as humans, ...

Evolution

EVOLUTION Evolution is  a change in the genetic composition of a population...

Genetics

Genetics is the study of heredity and variationHeredity- is the passage of chara...

Chat Icon Close Icon

Subscribe

×
Cancel