Comment

Topic

Ufahamu

Estimated reading: 4 minutes 101 views

Summary: Ufahamu ni dhana inayorejelea kujua na kulielewa jambo kwa usahihi na kuweza kulielezea upya kwa usahihi bila kupoteza maana yake ya msingi. Ufahamu wa mtu waweza kupimwa katika kusikiliza jambo au katika kusoma.

Kiswahili Kidato cha Kwanza

Jedwali la Yaliyomo

  1. Kusikiliza
  2. Kusoma kwa Sauti
  3. Kusoma Kimya
  4. Kusoma kwa Burudani

Kusikiliza

Ufahamu wa Kusikiliza

Ufahamu wa kusikiliza ni zaidi ya kusikiliza tu kile kilichosemwa; badala yake ni uwezo wa mtu kuelewa maana ya maneno anayoyasikia na kuweza kuhusiana nayo kwa namna fulani. Kwa mfano, mwanafunzi anaposikiliza hadithi, ufahamu mzuri wa kusikiliza humsaidia kuielewa hadithi hiyo, kuikumbuka, kuijadili, na hata kuisimulia tena kwa maneno yake mwenyewe.

Mambo ya Kuzingatia katika Ufahamu wa Kusikiliza

Ufahamu wa kusikiliza unahusisha michakato kadhaa katika kuelewa na kupata maana ya kile kinachozungumzwa. Michakato hii inahusisha:

  • Kuelewa vizuri sarufi ya lugha ile inayozungumzwa.
  • Kuelewa vyema maana ya maneno ya mhusika anayezungumza.
  • Kuelewa sintaksia (muundo wa maneno) ya sentensi kwa namna zinavyowasilishwa.

Katika ufahamu wa kusikiliza, msikilizaji hana budi kuzingatia mambo yafuatayo:

  • Kuwa makini: Elekeza akili yote kwa mzungumzaji ili kuweza kusikia kila anachokisema.
  • Vidokezo vya maana: Kutilia maanani vidokezo vya maana ili kubaini iwapo msemaji anaongeza jambo jipya, anatofautisha, anafafanua au anahitimisha hoja.
  • Kuandika mambo muhimu: Andika baadhi ya mambo anayoona kuwa ni ya muhimu ili kumasidia kukumbuka hapo baadaye.
  • Ishara za mwili: Kuwa makini na ishara mbambali za mwili kama vile kurusha mikono, kutingisha kichwa, kutingisha mabega au hata kupepesa macho. Ishara hizi huwa zinachangia kwa kiasi kikubwa kupata maana katika mazungumzo.

Kujibu Maswali kutokana na Habari uliyosikiliza

Jibu maswali kutokana na habari uliyosikiliza.

Activity 1

Jibu maswali kutokana na habari uliyosikiliza.


Kusoma kwa Sauti

Kusoma kwa sauti ni namna ya kuyaangalia maandishi na kuyatamka kwa sauti inayosikika.

Mambo ya Kuzingatia katika Ufahamu wa Kusoma

Kuna vipengele viwili vinavyounda mchakato wa ufahamu wa kusoma:

  • Uelewa wa msamiati: Uwezo wa kuelewa msamiati uliotumika katika matini hiyo. Endapo maneno yaliyotumika hayataeleweka, matini yote haitaeleweka.
  • Uelewa wa matini: Ili kuelewa habari/matini, msomaji anatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo:
    • Mawazo makuu: Kubaini mawazo makuu; msomaji anaposoma habari fulani au kitabu, inatakiwa ajiulize, “Je, kinachoongelewa hapa ni nini? Ni jambo gani hasa analolizungumzia mwandishi?” Maswali haya akilini mwake yatamsaidia kuelewa habari hiyo.
    • Alama za uakifishi: Kuzingatia alama za uakifishi; kwa kufanya hivyo, itamsaidia kuelewa ujumbe wa habari hiyo na endapo hatazingatia alama za uakifishi, anaweza kupotosha maana ya mwandishi.
    • Maana ya maneno na misemo: Kubaini maana ya maneno na misemo mbalimbali; habari nyingine huwa zina maneno ya kisanaa, hivyo ni muhimu msomaji kubaini maana ya maneno hayo katika muktadha wa habari hiyo, itamsaidia kuelewa vyema maana ya mwandishi.
    • Kumakinikia: Msomaji anatakiwa kumakinikia kile anachokisoma, kila kipengele anachokisoma inampasa akielewe vizuri.

Kwa kuzingatia haya yote, msomaji atakuwa na uelewa mzuri juu ya habari aliyoisoma na pia anaweza kufupisha habari hiyo aliyoisoma.

Kujibu Maswali kutokana na Habari uliyosoma

Jibu maswali kutokana na habari uliyosoma.

Activity 2

Jibu maswali kutokana na habari uliyosoma.


Kusoma Kimya

Katika usomaji huu, msomaji hufumba kinywa na kupitisha macho katika kila mstari haraka haraka. Macho hayo huunganisha neno lililotangulia na lile linalofuata. Ubongo wake huchambua mambo muhimu yanayojitokeza, huku akiyahifadhi kichwani. Mtu akijizoeza kusoma kimya, ananufaika ifuatavyo:

  • Hupata nafasi ya kupima mwendo wake na kiasi cha welewa.
  • Hujiepusha na lawama ya kusumbua wengine.
  • Hukwepa kuzingatia kanuni za matamshi.
  • Huweza kusoma maandishi mengi kuliko ambavyo angesoma kwa sauti.

Kujibu Maswali kutokana na Habari uliyoisoma

Jibu maswali kutokana na habari uliyosoma.


Kusoma kwa Burudani

Huu ni usomaji ambao lengo lake kuu huwa ni kujiburudisha tu. Katika usomaji wa aina hii, msomaji hujisomea zaidi magazeti, majarida, na vitabu tofauti na vile vinavyotumika darasani.

Mambo ya Kuzingatiwa katika Ufahamu wa Kusoma kwa Burudani

Wakati mwingine sio lazima msomaji awe na vitabu vyote ambavyo anahitaji kuvisoma au magazeti na majarida. Inapotokea hivyo, msomaji anaweza kwenda maktaba kuazima kitabu anachokihitaji.

Ingawa lengo la msomaji huwa ni kujiburudisha tu, lakini pia hujiongezea maarifa. Hii ni kwa sababu, magazeti, majarida, na vitabu, sambamba na kutumia lugha sanifu, huelezea mambo mbalimbali yanayoihusu jamii. Hivyo msomaji kutokana na kusoma vitabu na majarida mbalimbali hujiongezea kiwango cha welewa wa lugha na mambo mengine ya kijamii yanayojadiliwa humo.

Ni jambo zuri kwa msomaji kujijengea tabia ya kujipima ili aweze kuelewa kiwango cha maarifa aliyopata katika kujisomea. Kujipima huku kunaweza kufanywa kwa kujiundia utaratibu wa kuweka kumbukumbu ya vitu au makala zilizosomwa na kufanya ufupisho wa kila makala.

Utaratibu wa Kujipima na Kuweka Kumbukumbu

  • Tarehe: …
  • Jina la kitabu/makala/gazeti: …
  • Mchapishaji: …
  • Mwaka/tarehe ya uchapishaji: …
  • Ufupisho wa habari: (yasizidi maneno 20)
  • Fundisho/ujumbe mkuu ni: …
  • Jambo lililokuvutia sana: …
  • Maoni kwa ujumla kama yapo: …

Leave a Comment


Share this Doc

Ufahamu

Or copy link

CONTENTS

Translation And Interpretation | English Form 5 & 6

Translation is a process by which ideas that are written in one language ar...

Writing Skills | English Form 5 & 6

Are the abilities that allow you to write effectively and concisely. A competent...

Reading Skills | English Form 5 & 6

Reading is the process of going through written information or piece of wor...

Speaking Skills | English Form 5 & 6

What is Speaking? SPEAKING SKILLS: Speaking is simply the act of talking wh...

Listening Skills | English Form 5 & 6

Listening is ability to accurately receive and interpret messages in the communi...

Word Formation | English Form 5 & 6

This is the field or branch of morphology which studies different principles or ...

Introduction To Language | English Form 5 & 6

Language is a symbol system based on pure or arbitrary  conventions…...

Topic

Form Five and Form Six

Ecology

Ecology is the study of the interactions between living things, such as humans, ...

Evolution

EVOLUTION Evolution is  a change in the genetic composition of a population...

Genetics

Genetics is the study of heredity and variationHeredity- is the passage of chara...

Chat Icon Close Icon

Subscribe

×
Cancel