Comment

Topic

Kuongeza Msamiati Wa Kiswahili

Estimated reading: 3 minutes 125 views

Uundaji wa Maneno

Lugha hukua na kubadilika kila wakati kulingana na maendeleo ya jamii. Kigezo kimojawapo cha kukua na kubadilika kwa lugha ni kuongezeka kwa msamiati. Ili msamiati uongezeke katika lugha, sharti maneno mapya yaundwe.

Njia za Uundaji Maneno

Njia za Uundaji Msamiati hutokea kwa njia mbalimbali zifuatazo:

  1. Kubadili mpangilio wa herufi
  2. Kuambatanisha maneno
  3. Kutohoa maneno ya lugha nyingine
  4. Uambishaji wa maneno
  5. Kufananisha sauti, umbo, mlio na sura

Kuunda Msamiati kwa Kubadili Mpangilio wa Herufi

Neno hujengwa kwa vitamkwa au herufi. Neno jipya lenye maana tofauti huweza kuundwa kwa kubadili mpangilio wa neno lingine.

Mfano 1:

  • Neno “lima” lina herufi l, i, m, a. Herufi hizi huweza kujenga maneno kama mali, kumi, imla, mila.
  • Neno “tua” lina herufi t, u, a. Herufi hizi zinaweza kujenga maneno kama tatu, tua, viatu, tatua.

Njia ya Kuambatanisha Maneno

Kuna njia tatu za kuambatanisha maneno:

  1. Njia ya kurudufisha au kukariri neno
  • Mfano: barabara, sawasawa, polepole, katikati, vilevile.
  1. Njia ya uundaji wa msamiati kwa kuunganisha maneno mawili tofauti
  • Nomino na Nomino:
    • Punda + mlia = Pundamilia
    • Bibi + Shamba = Bibishamba
    • Afisa + Elimu = Afisaelimu
    • Mwana + Siasa = Mwanasiasa
    • Bata + maji = Batamaji
  • Kitenzi na Nomino/Jina:
    • Changa + moto = Changamoto
    • Chemsha + bongo = Chemshabongo
    • Piga + mbizi = Pigambizi
    • Zima + moto = Zimamoto
  1. Kuunganisha maneno mawili na kudondosha baadhi ya herufi
  • Mfano 2:
    • Baraza la Kiswahili Tanzania = BAKITA
    • Mzaliwa wa mahali Fulani = MZAWA
    • Chama cha Mapinduzi = CCM
    • Nyamamfu = NYAMAFU

Kutohoa Maneno Kutoka Lugha Nyingine

Kila lugha ina tabia ya kuchukua maneno kutoka lugha nyingine ili kukidhi mahitaji ya msamiati. Maneno yanapotoholewa kutoka lugha nyingine hubadilishwa kimatamshi ili yafuate kanuni za Kiswahili. Maneno haya husanifishwa na asasi za lugha ya Kiswahili kabla ya kutumiwa rasmi.

Mfano 3:

  • Neno la Kiswahili – Lugha ya Mwanzo – Neno Lililotoholewa
  • Shule – Kijerumani – Schule
  • Salama – Kiarabu – Salaam
  • Duka – Kihindi – Dukan
  • Karoti – Kiingereza – Carrot
  • Shati – Kiingereza – Shirt
  • Picha – Kiingereza – Picture
  • Papai – Kihispania – Papaya
  • Meza – Kireno – Mezi
  • Shukrani – Kiarabu – Shukran
  • Ngeli – Kihaya – Engeli
  • Ikulu – Kinyamwezi – Ikulu
  • Ng’atuka – Kizanaki – Ng’atuka
  • Ndafu – Kichaga – Ndafu

Kuunda Maneno kwa Njia ya Uambishaji wa Maneno

Hii ni njia ya kubandika viambishi awali na tamati kwenye kiini cha neno. Ujenzi wa maneno hutokana na mzizi mmoja kuonesha maana tofauti ingawa maana hizo zina husiana.

Mfano:

  • Mzizi: -lim-
  • Lima, analima, walilima, kilimo, limiana, halitalimwa, ukulima.

Kufananisha Sauti, Sura, au Tabia

Mfano 4:

  • Kengele – hutokana na sauti ya kengele inapopigwa.
  • Pikipiki – hutokana na muungurumo wa pikipiki.
  • Ndizi mkono wa tembo – Ndizi inayo fananishwa na mkono wa mnyama tembo.
  • Chubwi – Jiwe au chura atumbukiapo katika kina cha maji.

Mazingira Yanayoelezea Kuhitaji Maneno Mapya

Mabadiliko mengi yanatokea kila siku katika nyanja mbalimbali za kimaisha, kama vile mabadiliko ya kiuchumi, kisiasa, kisayansi, na kiteknolojia. Katika mazingira kama haya, watu watahitaji kuwasiliana na hivyo lugha itahitaji kuunda maneno mapya ili kuwasilisha dhana mpya zilizoibuka.

Mfano:

  • Maneno kama vile nywila, kisakuzi, udukuzi, puku, talakirishi yameundwa ili kuwasilisha dhana za kiteknolojia kwa Kiswahili.

Undaji wa Maneno katika Miktadha Mbalimbali

Mabadiliko ya kimaendeleo yanafanya lugha ihitaji maneno ya kuyafikisha na kutumiwa na jamii. Ili kukidhi mahitaji hayo, maneno mapya yanazuka. Maneno hayo yanaweza kuwa katika fani mbalimbali kama vile sayansi na teknolojia, siasa, utamaduni, na uchumi kulingana na mkondo wa maendeleo.

Mfano wa Msamiati:

  • Fedha, ushuru, kumpyuta, ukoloni, hospitali, suruali, n.k.

Activity 1: Unda Maneno katika Miktadha Mbalimbali

Tafadhali unda maneno mapya kulingana na mazingira yako. Fikiria maendeleo ya kiteknolojia, kisayansi, kiuchumi, na kisiasa na jinsi unavyoweza kuwasilisha dhana mpya kupitia maneno mapya ya Kiswahili.

Leave a Comment


Share this Doc

Kuongeza Msamiati Wa Kiswahili

Or copy link

CONTENTS

Translation And Interpretation | English Form 5 & 6

Translation is a process by which ideas that are written in one language ar...

Writing Skills | English Form 5 & 6

Are the abilities that allow you to write effectively and concisely. A competent...

Reading Skills | English Form 5 & 6

Reading is the process of going through written information or piece of wor...

Speaking Skills | English Form 5 & 6

What is Speaking? SPEAKING SKILLS: Speaking is simply the act of talking wh...

Listening Skills | English Form 5 & 6

Listening is ability to accurately receive and interpret messages in the communi...

Word Formation | English Form 5 & 6

This is the field or branch of morphology which studies different principles or ...

Introduction To Language | English Form 5 & 6

Language is a symbol system based on pure or arbitrary  conventions…...

Topic

Form Five and Form Six

Ecology

Ecology is the study of the interactions between living things, such as humans, ...

Evolution

EVOLUTION Evolution is  a change in the genetic composition of a population...

Genetics

Genetics is the study of heredity and variationHeredity- is the passage of chara...

Chat Icon Close Icon

Subscribe

×
Cancel